YAZID BIN MUAWIYAH BIN ABU SUFIYAN

Kimeandikwa Na: Sayyid Murtaza Rizvi

 

Babu yake Yazid, Abu Sufiyan ni miongoni mwa wale waliosilimu pasina budi ili kulinda mali zao na maisha yao katika Fat-hu Makka.  Kauli zake zathibitisha wazi kutokumuamini Mtume (s.a.w.w.).  Alimwambia Abbas “O Abbas! Kwa hakika mpwao amepata ufalme mkubwa” Abbas alimjibu “Ole wako! Huu si ufalme!  Huu ni Utume.” Rejea: (Tarekh Yakubi J. 2   Uk. 59.).

 

Baba yake Yazid, Muawiyah ni miongoni mwa wale waliompiga vita Imam Ali (a.s.) katika vita ya Swiffin.  Pia aliamrisha makhatibu kumlaani Imam Ali (a.s.) katika khutba za Ijumaa na Idd kwa muda wa miaka 80. Rejea: (Sahih Muslim J. 4   Uk. 1284 -  1285, na Hayatu Omar bin Abdul aziz Uk. 252.).

 

Bibi yake Yazid, Hinda ndiye aliyekula Ini la Sayyidina Hamza katika vita vya Uhud.Yazid alifuata nyayo za babu, bibi na baba yake katika imani na matendo.  Nae wazi wazi akiimba mashairi ya  kufru akisema: “Laibat Hashim bil mulki-falaa khabarun ja’a wala wahyun nazal” yaani: Banu Hashim walicheza mchezo wa kupata ufalme: kwa hakika hakukuwa na habari yoyote (kwa Mungu) wala wahyi wowote ulioteremshwa.” Rejea: (Tarekh Tabari J. 13 Uk. 2174.).

     

Yazid alitangaza wazi wazi kutomuamini Mtume (s.a.w.w.) na ujumbe wake.  Alichezea shere Imani ya siku ya malipo, alidhihaki sala, ulevi ulikuwa kinywaji chake, kamari kwake ni kawaida.  Alikuwa akizini mpaka na mama zake wa kambo na shangazi zake. Rejea: (Maruuju Dhahab J. 3  Uk. 77. na Al-Bidaya wan-nihayah J. 5  Uk. 746.).

     

Katika kipindi chake Yazid alifanya uharibifu mkubwa katika Dini.  Jeshi lilivamia miji mitukufu ya Makka na Madina.  Aliwaua wasomaji wa Qur’an 700 na pia aliwaua mamia ya Masahaba wa Mtukufu Mtume (s.a.w.w.). Na waliwazini wanawake kwa maelfu na kuuchafua msikiti wa Mtume (s.a.w.w.).  Mji Mtukufu wa Makka ulizingirwa na jeshi la Yazid na moto mkali uliwashwa kwenye Al-Kaaba na sehemu ya Al- Kaaba kuvunjika. Rejea: (Muruuju Dhahab J.3 Uk.    81.).

 
 

Prepared by: Khoja Shia Ithna Asheri Dar es Salaam Juloos Committee 1429AH (2008)
Email us your comments, suggestions, articles, etc through the Website Coordinator: Murtaza H. Lalji