Uislamu Ni nini?

Mwandishi:

Hujjatul Islam wal Muslimeen Al-Haj Sayyid Muhammad Rizvi     

Uislamu ni Dini inayowaongoza Waumini wake katika kila nyanja ya maisha yao. Ni mfumo wa maisha.

 

Uislamu ni mwongozo au Wahyi ulioteremshwa na Mwenyezi Mungu kupitia Mtume Adamu, Nooh, Abraham, Mussa na Issa (Yesu).

 

Uislamu uliletwa kwa Mwanadamu kupitia kwa Mtume Muhammad.  Uislamu ni “mwongozo” kwa maana kwamba umeletwa kuhakiki mafunzo yalioletwa kupitia kwa Mussa na {Yesu}Issa.

 

Uislamu ni Dini inayoelezea maana na kusudio la maisha yetu katika Ulimwengu huu.  Uislamu unatuongoza sisi katika kukidhi kusudio kwa kutengeneza mazingira ya uelewano baina yetu, Muumba wetu na Wanadamu.

 

Yafuatayo ni baadhi ya mambo ya msingi katika Uislamu.

 

MWENYEZI MUNGU NI MMOJA NA PEKE YAKE

Uislamu ni Dini inayoitakidi Mungu mmoja.  Uislamu unatufundisha kuwa Mungu ni mmoja na ndiye Muumba wa Ulimwengu.  Hili ndio jiwe la msingi la Uislamu na msingi huu umeelezewa katika usemi maarufu usemao:  “Hapana Mola isipokuwa Allah” (Allah ni jina la Kiarabu la Mola  jina hili linatamkwa  “Al-lah”).

 

Kuamini  Mungu inatufungamanisha sisi na utangu (mwanzo) wetu na kutuongoza katika maisha yetu yote.  Imani yetu  katika Mungu mmoja inatuashiria kuwa mwanadamu hatakiwi kuabudia kitu chochote au Binadamu yeyote katika Ulimwengu huu.  

 

Kwa kufundisha kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja kwa Wanadamu wote, Uislamu hueneza nadharia ya udugu na usawa katika jamii ya Wanadamu wote wanao uhusiano ulio sawa kwa Mwenyezi Mungu.  Qur’an {kitabu kitakatifu cha Kiislamu} inasema:-Yeye Allah ni (Mungu) mmoja tu.  Al-lah ni Mwenye kukusudiwa na Wahitaji wote.  Hakuzaa wala Hakuzaliwa. Wala hakuna hata mmoja mfano Wake. {Sura 112}.

 

KUSUDIO LA MAISHA

Maisha yetu katika ulimwengu huu yanayo makusudio maalum, na sio matokeo ya ajali ya asili wala  sio adhabu kwa kula tunda la mti uliokatazwa na Mwenyezi Mungu.  Tupo hapa kutokana na mipango yake Allah.  Maisha ya hapa Duniani ni majaribio, dhidi ya maisha ya Peponi baada ya maisha ya hapa {Duniani}.  Mwenyezi Mungu hakutuumba tu kwa ajili ya maisha ya miaka michache hapa Duniani.  Kuumbwa kwa ajili ya maisha ya hapa Duniani tu ingekuwa ni mzaha uliochezwa baina ya Muumba {Allah}na jamii ya Wanadamu.  Muhammad Mtume wa Uislamu amesema “Hujaumbwa ili ufe na kupotea bure ila {lakini}umeumbwa kwa ajili ya maisha ya milele.

 

Kulingana na Imani ya Kiislamu Kituo cha mwisho cha mwanadamu ni maisha ya hapo baadae {Akhera}.  Mwisho, wanadamu wote watafufuliwa na wataulizwa siku hiyo kuhusu matendo yao walipokuwa hapa Duniani. Maisha ya Akhera yatakuwa ni maisha ya milele.  Hata hivyo, maisha ya peponi au adhabu {Jahannam}itategemea ni vipi tutayatumia maisha yetu hivi sasa.  Kumsaidia mwanadamu afikie lengo hili Mwenyezi Mungu amewaleta Manabii na Mitume mbali mbali ili kuwaongoza.  Muhammad ni Nabii wa mwisho na Uislamu ni Wahyi wa mwisho wa ujumbe wa Allah uliokamilika.

 

HADHI YA MWANADAMU KATIKA UISLAMU

Kiumbe Bora:  Mwanadamu ni kiumbe bora cha Mwenyezi Mungu.  Mwenyezi Mungu amesema:  “Na hakika tumewatukuza Wanadamu na tumewapa vya kupanda barani na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewatukuza kuliko wengine katika wale tuliowaumba, kwa utukufu ulio mkubwa kabisa”. {Qur’an 17:70}

 

Tumezaliwa bila dhambi: Uislamu unatufunza kuwa kila mwanadamu huzaliwa bila dhambi {takatifu} hakuna kizazi kinachobeba mzigo {madhambi} ya mababu {wahenga} zao.  Allah {s.w.t.}anasema;  Wala hatabeba mbebaji mzigo wa mwingine {kila mtu atachukua jukumu la dhambi zake mwenyewe}  Surah 35 Ayah 18. Kila mwanadamu anazaliwa akiwa safi (bila dhambi:) akiwa tayari kuupokea ujumbe wa Al-lah.  Ni mazingira ya kijamii na kifamilia yanayomtoa mwanadamu nje ya ujumbe wa Allah.

 

Uwajibikaji: Uislamu pia unasisitiza suala la majukumu na uwajibikaji kwa wanadamu-kila mmoja anawajibika kwa  vitendo vyake mwenyewe.  Ingawa Uislamu unatufunza kuwa A-l lah{s.w.t.}amesha weka tayari mwenendo wa maisha  yetu na wakati wakifo, hii haina maana kuwa hata vitendo vyetu vimepangwa na Allah {s.w.t.}.  Hakika tupo huru na vitendo vyetu, hivyo tunawajibika navyo.  Mwenyezi  Mungu ametoa mwongozo tu, kwa mwanadamu kujua lipi jema na lipi baya.  Mwenyezi Mungu amesema: “Hakika sisi tumemuongoa {tumembainishia} njia {zote mbili hizi, kuwa hii ndio ya kheri na hii ndio ya shari}.  Basi {mwenyewe tena}atakuwa mwenye shukurani au awe mwenye kukufuru, {kukanusha}. {Qur’an Surah 76:3}.

 

Uraia {Ukabila}: Uislamu unakataa unyanyasaji wa kikabila kwa misingi yoyote ile. Uislamu unafundisha misingi ya udugu na usawa miongoni mwa  waumini wake. Allah {swt}anasema wazi wazi:

 

“Enyi watu! Kwa hakika tumekuumbeni {nyote} kwa {yule} mwanamume mmoja;  Adamu} na {yule yule} mwanamke {mmoja; Hawwa}. Na tumekufanyeni mataifa na makabila {mbalimbali} ili mjuane {tu basi;sio mkejeliane}.”   Allah anaendelea kusema; Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule amchae Mungu zaidi katika nyinyi.  Kwa yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, mwenye habari {za mambo yote}. {Qur’an 49:13}.

 

Jinsia: Hata jinsia haiwezi ikamweka mtu katika ubora.  Katika Uislamu Wanawake ni Wanadamu kama wanaume.  Hawa tengwi kwa misingi ya jinsia yao; isipokuwa kwa misingi ya Imani na vitendo vyao.  Miaka 1400 iliyopita Qur’an imeeleza wazi ujumbe wa Allah kuhusu suala hili.   Zipo Aya nne zinazoelezea suala hili, hapa nanukuu Aya moja:  “Na watakao fanya vitendo vizuri, wakiwa wanaume au wanawake hali wao ni wenye kuamini basi hao wataingia Peponi wala hawata-dhulumiwa hata tunda ya kokwa ya tende”.  {Qur’an 4:124}

 

Hivyo hakuna tofauti katika daraja au ubora wa utu wa mwanamume au mwanamke mbele ya Uislamu.

 

Ubora  pekee unaopatikana hapa unahusu kiwango na upeo jinsi Uislamu ulivyopokewa na mwanamume na mwanamke.  Katika Uislamu, mwanamume na mwanamke wapo sawa katika haki, lakini usawa huo haubaki hivyo katika vitendo vyao.  Uislamu unaamini kuwa mwanamume na mwanamke wako sawa, lakini hawafanani kw vitendo vyao.  Uislamu naangalia tofauti ya majukumu yao  katika Jamii kuwa sio makubwa wala madogo lakini yenye yenyekutegemeana.

 

 

UISLAMU DINI YA AMANI

Uislamu ni dini ya Amani.  Hii inathibitishwa hata katika jina  “Isalmu”.  Jina lenyewe {“Islamu ni neno la Kiarabu} Jina  “Islamu” ni neno la Kiarabu la amani “Salam” yote mawili yanatokana na asili moja “Salima”.

 

Waislamu wanafundishwa kusalimiana kwa kusema “Salamun alaykum-amani iwe juu yako”.  Sala za  kila siku pia humalizia kwa maneno hayo.  Katika Uislamu, miongoni mwa majina ambayo Mwenyezi Mungu huitwa ni “Salam” ikiwa na maana ya “amani”.

 

Hata hivyo mtu lazima atambue kuwa amani haiwezi kupatikana kwenye sehemu tupu {isiyo na kitu}.  Lazima iunganishwe na haki. Mtu anaweza kupata amani tu, katika misingi ya haki.  “Haki” maana yake kuweka kila kitu katika nafasi yake.  Iwapo mtu ataanza kuweka vitu katika sehemu isiyohusika ataukera utulivu wa jamii na kuvunja amani.  Uislamu huhifadhi amani katika nyanja mbili.

 

1.   Amani ya Mtu binafsi:  Mtu hupata amani yake binafsi kwa kuwa mtulivu na kuwa na uwiano wa mwenendo {matamanio na hasira} na matendo ya kiroho.

 

Nguvu ya kiroho ya mwanadamu haina utulivu uliojitosheleza; inayo uwezo wa kukuwa na pia kuvia.  Mwenyezi Mungu anaapa kwa moyo wa mwanadamu na anasema:- “Bila shaka amefaulu aliyeitakasa {nafsi yake}Na bila shaka amejihasiri aliyeiviza nafsi yake” {Qur’an  91:10}.

 

2.   Amani na Wanadamu wengine: Uislamu umesisitiza kwa nguvu zote juu ya haki ambazo watu wengine wanazo juu ya wengine.  Uislamu unahubiri amani katika jamii kwa kuwafunza na kuwataka Waumin wake kutekeleza haki zao baina yao.  Katika Uislamu wokovu haupatikani kwa kutekeleza Haki za Allah tu.  Muumini atatakiwa kutekeleza haki za Wanadamu wengine pia.  Kwa bahati mbaya kutokana na matukio ya Mashariki ya kati kwa muda wa ¾  ya karne, Uislamu umepewa jina na vyombo vya habari kuwa ni Dini ya ghasia {mapambano}, katika miaka ya karibuni neno “Uislamu” limekuwa miongoni mwa sifa za “Ugaidi”.

 

Katika hali hii kwanza lazima mtu atambue kuwa matukio ya Mashariki ya Kati yanaweza kufahamika vema tu kwa msaada wa kihistoria wa vita kuu ya kwanza ya eneo hilo, hususan ahadi zilizotolewa na Wazungu kwa Waarabu.  Pili hakuna mtu mwenye akili timamu angethubutu mwenyewe kuilaumu Dini ya Kiislamu kwa matendo maovu ya wale wanaojiita Waislamu.  Hii ni kama kusema Kanisa Katoliki linazua ghasia na Ugaidi kwa sababu ya shughuli za Jeshi la  “Irish Republican”.

 

Je, unafahamu kwamba:-

*  Kila watu watano Duniani, mmoja ni Mwislamu?

*  Waislamu walio wengi sio Waarabu wa raia wa Uarabuni?

*  Wapo Waislamu million 4.6 U.S.A.?

*  Uislamu ni Din inayo enea kwa haraka zaidi U.S.A.?

* Je! huu si wakati muafaka kwako kujikurubisha na Uislamu?

 

Ewe Allah tuangazie  juu  yetu mwanga wa Elimu na Utuondoe kutoka kwenye giza  la  ujinga.

 

Ijaze mioyo yetu kwa Elimu  na Hekima.

 

Ijaalie Elimu yetu iwe ya manufaa kiroho.  Tujaalie mafanikio katika kujua na kuuhami Uislamu. AMEEN!

 
 

Prepared by: Khoja Shia Ithna Asheri Dar es Salaam Juloos Committee 1429AH (2008)
Email us your comments, suggestions, articles, etc through the Website Coordinator: Murtaza H. Lalji