Ujumbe wa Siku ya Ashura

kutoka kwa

Ayatullah Al-Uzma Mirza Jawwad Tabrezi (Qum-Iran).

 

Katika Mji mtakatifu wa Qum, Irani; Ayatullah Al-Mirza Jawwad At -Tabrezi ameelezea rambirambi zake za dhati kwa wafuasi wa Aal-e-Muhammad (a.s.) kwa tukio hili linalowagusa la masaibu ya Karbala.

 

Katika ujumbe wake kwenye tukio la siku ya Ashura, mtukufu Ayatullah At-Tabrezi alisema kifo cha Bwana wa Mashahidi Hazrat Aba Abdillah Al-Hussain (a.s.) ni njia inayong’ara na itoayo mwanga kwa Waumini, wapigania Uhuru, wanaonyanyaswa na kwa kila tabaka la jamii na pia kwa Dini na Imani zote.

 

Ayatullah alisema kuwa fundisho linalopatikana katika tukio hili la huzuni ni kuwa ushindi kati ya Haki na Batili wakati wote upo pamoja na Haki (ukweli).

 
 

Prepared by: Khoja Shia Ithna Asheri Dar es Salaam Juloos Committee 1429AH (2008)
Email us your comments, suggestions, articles, etc through the Website Coordinator: Murtaza H. Lalji