|
UTUKUFU WA IMAM HUSSEIN BIN ALI BIN ABI TALIB (A.S.)
Kimeandikwa Na:
Sayyid Murtaza Rizvi
Imamu
Hussein ni katika wale ambao Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewatoharisha na
kuwatakasa na machafu kama ilivyo katika Qur’ani Tukufu Sura ya 33:33.
Imepokewa kutoka kwa Ummu-Salama (mke wa Mtume) kwamba ilipoteremka
Aya hii ya utakaso (33:33) ndani ya nyumba yangu, nikiwa mlangoni pamoja
na Mtume na Ali, Fatimah, Hassan na Hussein pamoja na Malaika Jibril na
Mikail wakiwa ndani ya nyumba yangu, nilisema:-
“Ewe Mtume!
Je! Mimi si katika Ahlul –Bayt wako?. Mtume (s.a.w.w.) akasema,”
Hakika wewe Ummu Salama u katika kheri na wewe ni katika wake za Mtume
(s.a.w.w.). Rejea: (Durrul Manthur- Juzuu ya 6, Uk. 604-605. na
Tafsiri Tabari Juzuu ya 10, Uk. 298 na Tafsiri Ibn Kathir
Juzuu ya 3, Uk. 531).
Iliposhuka
Aya ya Mawaddatul-Kurba (Sura ya 42:23), Mwenyezi Mungu alimwambia Mtume
(s.a.w.w.) katika Qur’an tukufu awaambie Ummah wake hivi:- “Qul laa
as-alukum alayhi ajran il-lal Mawaddata fil-Qurbaa” waambie siwataki
malipo yoyote juu ya (Utume niliokuja nao) ila mapenzi juu ya Aqraba
wangu (42:23). Mtume (s.a.w.w.) aliulizwa, hawa Mawaddatul-fil Kurba
(Aqraba) ni nani na akajibu ni watu wa nyumba yake yaani Ahlul-Bayt. Aya
hii inaweka wazi kuwa kuwapenda Ahlu-Bayt wa Mtume ni wajibu usio shaka
juu ya kila Muislamu. Rejea: (Tafsiri Ibn Kathir Juzuu ya 4, Uk.
121-123. na Fathul Qadiir Juzuu ya 4, Uk. 760. na Tafsiri
Tabari Juzuu ya 11, Uk. 142-145. na Durrul Manthur- Juzuu ya 7,
Uk. 348-349.).
Ilipoteremshwa Aya ya kuapizana yaani “Mubahala” alipoambiwa Mtume
(s.a.w.w.) Sema; Njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu na wake zetu
na wake zenu na nafsi zetu na nafsi zenu, kisha tuapizane. Mtume alitoka
na Sayyidna Imam Hassan na Imam Hussein (watoto wake) Bibi Fatima (mke
wa Imam Ali bin Abi Talib), Mtume (s.a.w.w.) na Sayyidna Imam Ali (Nafsi
zetu). Makafiri wa Najran walipomuona Mtume (s.a.w.w.) na nyuso za wale
watukufu na watoharifu Ahlul-Bayt wa nyumba ya Mtume (s.a.w.w.)
walikataa kuapizana na badala yake walikubali kulipa jizya (kodi).
Rejea: (Ruhul-Maan J. 2 Uk. 180-181. na Fadhul-Qadiyr J. 11
Uk. 524. na Durrul- Manthur J. 2 Uk. 232-233.).
Mtume
(s.a.w.w.) amesema: “Ewe Mola! Mimi nampenda Hussein nawe mpende,
Hussein anatokana na mimi na mimi ninatokana na Hussein, umpende mwenye
kumpenda (Hussein)”. Rejea: (Sahih Muslim J. 4 Uk. 1293.). Na
vile vile Mtume (s.a.w.w.) amesema: “Hasan na Hussein ni mabwana wa
vijana wa Peponi, anipendae awapende hawa wawili”. Rejea: (Sawaiqul
Muhriqa Uk. 522.).
Kuwasalia
Aali Muhammad ni nguzo ya Sala na kuacha kuwasalia wao ni kuibatilisha
Sala. Rejea: (Sawaiqul Muhriqa Uk. 147.).
Pia amesema
Bwana Mtume (s.a.w.w.): “Hakika Mfano wa Ahlul Bayt wangu kwenu ni mfano
wa Safina ya Nabii Nuh (a.s.) waliopanda Safina hiyo waliokoka na wale
waliokataa kupanda Safina hiyo waliangamia.” Rejea: (Sawaiqul Muhriqa
Uk. 150.).
Na mwisho ni
kauli ya Imam Shafi aliposema: “Ikiwa dhambi yangu ni kuwapenda watoto
wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.) [Imam Hassan na Imam Hussein] basi ni
dhambi ambazo sitatubia”.
|