|
Ujumbe wa Siku ya Ashura
kutoka kwa Ayatullah Al-Uzma Sayyid Muhammad Saeed Al-Hakim (Najaf-Iraq)
Siku ya
Ashura hutonesha majeraha yetu, na hupelekea macho yetu kububujikwa na
machozi kutokana na vipenzi vyetu kuuliwa mashahidi katika ardhi ya
Karbala, na kutuweka katika usumbufu na majuto hadi siku ya Hisabu (Kiyama).
Hivyo, huyu ni Husain (a.s.) ambaye watu wapaswa kumlilia (na kuomboleza)
kwa kuuliwa shahidi.(Imam Ali Raza (a.s.)).
Sisi na
ndugu zetu wote tunakumbuka (mahali hapa) katika siku hizi maalumu za
matukio ya Imam Husain (a.s.), pia Mapinduzi ya Kiislamu katika nyanja
zote yakiongozwa na Imam Husain (a.s.), Ahlul Bayt wake, Mashaba,
Wanamume, Wanawake, Wazee, Vijana na Watoto kwa upande mmoja na matendo
ya kikatili yaliyotendwa na Madhalimu wa mauaji haya kwa upande mwingine.
Tunapenda
kuziangalia baadhi ya nukta ili tupate mafunzo kutoka kwenye ujumbe wa
Imam Husain (a.s.), uliotikisa utawala wa Madhalimu katika kila zama na
kuuhuisha Uislamu kwa faida ya kizazi kijacho.
Ili kupata mafanikio katika wakati huu mambo yafuatayo yapaswa kufuatwa:
-
* Kuonyesha
majuto na huzuni kufuatana na mwenendo wa Ahlul Bayt (a.s.). Katika
Hadithi yake Imam Raza (a.s.) anasema “Mwanzoni mwa mwezi wa Muharram,
baba yangu alikuwa hacheki na alionekana amejawa na huzuni mwezi mzima
na ilipowadia siku ya kumi ya Mwezi wa Muharram, siku ya usumbufu,
matatizo na maombolezo alisema “ Hii ni siku ambayo Imam Husain (a.s.)
aliuliwa (kikatili)”.
* Kujiandaa
na kushiriki katika Aza (maombolezo) ya Imamu Husain (a.s.) katika
Misikiti, Husainia, n.k. kwa kuwa matendo haya ni utukufu wa alama za
Allah (s.w.t.) kama Qur’ani inavyosema: “Namna hivi, anayeziheshimu
alama za (dini ya) Mwenyezi Mungu, basi hilo ni jambo la Utawala (ucha
Mungu) wa nyoyo” (Hajj:32).
|