|
MUHANGA MKUBWA WA IMAM HUSSEIN (A.S.) IMETABIRIWA NDANI YA BIBLIA NA
QUR’ANI
Hata Biblia nayo imetabiri kifo cha Imam Hussein (a.s.) kwa kutaja
hivi:-
“Maana hiyo ni siku ya BWANA, Bwana wa Majeshi, siku ya kisasi, ili
ajilipize kisasi juu ya adui zake; Nao upanga utakula na kushiba,
utakunywa damu yao hata kukinai, maana Bwana, BWANA wa Majeshi,
anasadaka yake katika nchi ya Kaskazini karibu na mto Frati.” Rejea: (AGANO
LA KALE; JEREMIA 46:10.).
Hata Qur’ani nayo imetabiri
kifo cha Imam Hussein (a.s.), Hii ni ‘Zibhe-Azeem’ au Muhanga Mkubwa,
ambao Mungu ameutabiri kuchukuwa mahali pa Muhanga wa Idrahim: - “Ewe
Ibrahim! Umekwisha itimiiza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo
walipa wanao tenda mema, Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri, Basi
tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu, Na tukamwachia kwa watu walio kuja
baadaye.” (Qur’ani Tukufu; 37: 105-108).
|