|
BUSTANI YA USEMI
“Yeyote awapendaye Hassan na Husein amenipenda, na yeyote anayewachukia
amenichukia.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“…., Allăh hujirafikisha na wale wajirafikishao na Husain yu adui wa
wale walio maadui zake.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
Husain anatokana na mimi na mimi ninatokana na Husain…”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
Hao (Hassan na Husain) ni maua yangu katika dunia.”(Ewe Husain), wewe u
Sayyid, mwana wa Sayyid, na ndugu wa Sayyid; wewe uthibitisho (wa
Mwenyezi Mungu) na mwana wa uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu) na ndugu wa
uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu); na baba wa uthibitisho tisa ambao wa
tisa wao ni Qaim wao ambaye atakuwa Al-Mahdi.
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
Ewe mwanangu (Husain)! Mwili wako ni mwili wangu na damu yako ni damu
yangu.
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“Ewe Mola wangu! Mpende yule ampenda Husain.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“Hassan na Husain ni masayyidi wa vijana wa peponi.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“Adhabu atakayoipewa yule mwuaji wa Husain huko Motoni itakuwa sawa na
nusu (nzima) ya adhabu yote watakayoipewa wenye dhambi waulimwengu.”
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“Yeyote awapendaye Hassan na Husein amenipenda, na yeyote anayewachukia
amenichukia”.
Mtukufu Mtume (s.a.w.w.)
“Kufa kwa heshima ni bora kuliko kuishi kwa aibu”
Imăm Husain (a.s.)
“Kama Dini ya (Mtume) Muhammad (s.a.w.a.) haiwezi kuendelea ila kwa
kukitoa mhanga kichwa changu, basi upanga na uje ukichukue.”
Imăm Husain (a.s.)
Imăm Hassan na Imăm Husain (a.s.) wameuhurisha Uislamu kutokana na
utumwa wa wafalme na hivyo basi, wameuhifadhi kutokana na uharibifu
daima. wafalme watakuja, na wafalme watakwenda, lakini Uislamu utadumu
milele. Kwa Uislamu, majina matakatifu ya Hassan na Husain yataangaza
milele.
Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi (r.a.)
Katika mambo yenye kunikesheza na kuzifanya nyeupe nywele zangu ni
huzuni na misiba ya kilimwengu.
Imăm Shafii (r.a.)
Huzuni yangu imenirudia na moyo wangu unahuzuni. Jicho langu halifumbi
wala usingizi siujuwi.
Imăm Shafii (r.a.)
Kwa sababu ya Ahli-Bayt ya Mtume (s.a.w.a.), Ulimwengu mzima ulitetema
na majabali na milima ilikaribia kuyayuka.
Imăm Shafii (r.a.)
Ni nani atakae mfikizia Hussein ujumbe wangu na hata kama nyoyo zatukia?
Imăm Shafii (r.a.)
Hussein! Aliuliwa shahidi pasi na makosa yoyote na kanzu yake
ikatapakazwa wekundu.
Imăm Shafii (r.a.)
Twamuombea rehma Mtume katika ukoo wa Hashim na twawaudhi wanawe; hakika
jambo hilo ni lenye kustaajabisha.
Imăm Shafii (r.a.)
Ikiwa dhambi zangu ni kuwapenda watoto wa Mtume Mohammad (s.a.w.) basi
ni dhambi ambazo sitatubiya.
Imăm Shafii (r.a.)
Kuwa ni wao ndio watakao nishufaiya siku ya kufufuliwa na hisabu, na
mwenye kuwabugudhi wao ni wenye dhambi kwa Shafii.
Imăm Shafii (r.a.)
Husain ni Mfalme (ni Bwana) Husain ni Mfalme wa Wafalme (ni Bwana wa
Mabwana); Husain ni Dini, Husain ndiye mhifadhi wa Dini. Kichwa
alikitoa, bali hakutoa mkono wake juu ya mkono wa Yazid; Hakika Husain
ndiye msingi wa Lailaha illallah.
Khwaja Muienuddin Chishti Ajmeri (r.a.)
|