SHAHIDI WA KARBALA
SAYYIDINA IMAM HUSSEIN BIN ALI BIN ABI TALIB (A.S.)
Kimeandikwa Na: Sayyid Murtaza Rizvi

 

10 Muharram ni siku ya Ashura, Miaka 1364 iliyopita siku ambayo mjukuu wa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w.), Sayyidina Imam Hussein, mtoto wa Imam Ali bin Abi Talib (a.s.) na mama Fatimah bint Muhammad (s.a.w.w.), mrithi wa tatu wa haki wa Mtume wa Uislamu, mrithi wa Adam, Nuh, Ibrahim, Musa, Isa, Muhammad na Ali, aliuliwa kikatili na Yazidi bin Muawiyya bin Abu Sufyan baada ya kukataa kutoa kiapo cha utiifu kwa Yazid.

Siku hii ni kumbu kumbu ya kujitoa muhanga kwa Imam Hussein (a.s.) katika kuinususru Dini na kuitetea haki, dhidi ya wapinzani wa Uislam.  Sababu kubwa ya kuuliwa Imam Hussein ni kukataa dhuluma na uongo, na kutaka kusimamisha Haki na Ukweli kama babu yake Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alivyoamrisha. Tukio hili halikuwa la kawaida kwani Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alishabashiri wakati aliposema: “Kwa hakika kifo (shahada) cha (Imam) Hussein kitaamsha mori katika nyoyo za Waumini ambao hazitopoa milele.” Rejea: (Mustadrak: J. 11, Uk. 27)

Siku hii, mamilioni wa Waumini Duniani kote wanaomboleza kifo cha Imam Hussein (a.s.) kiigizo cha kweli cha Mtumishi wa Allah (s.w.t.) muamarishaji nguvu za jeshi la Mungu dhidi ya majeshi ya Shetani, tukiangalia historia ya Kiislam tunaona kuwa umma ulikwenda kinyume na maamrisho na mafundisho ya Mtume (s.a.w.w.) ambayo alitaka tushikamane nayo. 

Imam Hussein alikuwa ni kizito cha pili kati ya vizito alivyotuamrisha Mtume (s.a.w.w.) tushikamane navyo, kama Mtume mwenyewe alivyosema “Enyi watu! Hakika mimi ninakuachieni vityu viwili vizito ambavyo mkishikamana navyo hamtapotea milele, navyo ni kitabu cha Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Qur’ani na kizazi changu yaani Ahlul-Bayt (a.s.)”. Rejea: (Tirmiz-Juzuu ya 5, Uk. 433. na Riyadhus-Salihiyn, Uk. 165, Babu Ikrami Ahlul-Bayt).

 

 
 

Prepared by: Khoja Shia Ithna Asheri Dar es Salaam Juloos Committee 1429AH (2008)
Email us your comments, suggestions, articles, etc through the Website Coordinator: Murtaza H. Lalji